Hapo mwanzo, mwanamume na mwanamke walikuwa katika nafasi
sawa mbele za Mungu. Lakini wakati Hawa alipoanguka katika kosa baada ya
kumsikiliza nyoka, agano lilibadilishwa. Mwanamke huyo sasa alikuwa chini ya
utii kwa mwanaume, kama tu inavyojidhihirisha katika Maandiko yafuatayo:
1Thimotheo
2:14-15 “Wala Adamu
hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa
kabisa akaingia katika hali ya kukosa. Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa
kiasi.”
Mwanzo 3:16
“Akamwambia mwanamke, Hakika
nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako
itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.”
Waefeso
5:22-24 “Enyi wake, watiini waume
zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa
maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye
ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile
Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.”
Nabii Isaya
alikuwa akihukumu Israeli wakati
aliposema kwamba wanawake wanatawala juu yao (Isaya 3:12). Nabii Eliya pia alikuwa akimhukumu Ahabu kwa sababu mke wake wa kipagani Yezebeli alikuwa akimtawala. Samson
aligeuka nje ya mapenzi ya Mungu kwa sababu alisikiliza maagizo ya Delila. Na Adamu mwenyewe alishindwa katika Mungu kwa sababu ya kumsikiliza
mkewe Hawa.
Katika kanisa, kulingana na Biblia, hakuna mwanamke
anayestahili kuwa mchungaji au shemasi au kushika nafasi nyingine yoyote ya
uongozi dhidi ya wanaume. Nani anasema hiyo? Mungu mwenyewe alisema kupitia
kinywa chake cha Agano Jipya, mtume
Paulo.
1Timotheo 2:
11-15 inasema wazi:
“Mwanamke na
ajifunze katika utulivu, akitii kwa
kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya
kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu. Kwa maana
Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia
katika hali ya kukosa. Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu
katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.”
1Wakoritho
14:34-37 inasema;
“Wanawake na
wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile
inenavyo torati nayo. Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume
zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.”
Je! Mwanamke anawezaje kuwa mchungaji wa
kanisa wakati yeye amekatazwa kufundisha au kuwa na mamlaka yoyote juu ya
wanaume?
Wanawake wanaweza tu kuwa wachungaji ikiwa makanisa
yanakataa kwa makusudi na kwa uwazi mafundisho ya Biblia. Kwa bahati mbaya, makanisa leo, hata
Wapentekoste, mara nyingi wameambukizwa na tabia ya kidunia. Ukombozi wa Wanawake umevamia makanisa (kile
wanaita haki sawa). Kwa hivyo, uasi wa
wanawake ulimwenguni unazua matatizo sawa na hayo katika makanisa, na tunapata
wanawake wakitamani na kudai nafasi za uongozi katika makanisa mengi.
Mungu ni mwanamume, na kanisa ni mwanamke. Kwa hiyo, mwanamke anapaswa kumtii mwanamume
kama vile kanisa lilivyo chini ya Kristo, na si kinyume chake.
WANAWAKE
KATIKA HUDUMA 5?
SUALA
KUU linaweza kufupishwa kama ifuatavyo: “Je! Mwanamke anaweza kuwekwa wakfu kwa
huduma ya kichungaji?”
Ikiwa
unaamini Biblia, jibu ni HAPANA thabiti!
Biblia inazungumza
kwa uwazi sana juu ya somo hili bila kuacha nafasi ya uvumi na kuchanganyikiwa,
au hata mjadala. Tatizo ni kwamba
makanisa leo mara nyingi sana yanatafuta vyanzo vingine badala ya Biblia ili
kuhalalisha imani zao zisizo na maana.
Matokeo yake ni kulewa kwa mawazo yanayopinga mamlaka ya Maandiko.
Ingawa wanawake wanaweza kuhudumu kanisani katika nyadhifa
mbalimbali mradi tu uwezo huo haukiuki kanuni za mamlaka na utaratibu na uongozi wa kiume, basi hiyo ni sawa. Wanawake wanaweza kuwa na mamlaka ya kiroho
juu ya wanawake wenzao na watoto lakini si juu ya wanaume.
Sipuuzi ukweli kwamba kuna wanawake wengi ambao wana uwezo
mkubwa. Lakini ni muhimu kukumbuka kuwa
suala hili halihusiani na thamani au
uwezo. Inahusiana na maagizo na mamlaka. Mungu ameweka
kitengo cha familia, na Kanisa lenyewe, katika utaratibu ufaao.
1Wakoritho 14:40 inasema; “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.” Waebrania 13:17 “Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea;
maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili
kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.”
Wanawake wanaweza kutumika kwa matokeo mazuri kanisani hata
hivyo si kama Wachungaji, Wazee au Mashemasi. Yesu alichagua wanaume kumi na wawili kuwa
viongozi wa msingi wa Kanisa Lake, na mitume waliamriwa kuchagua wanaume saba
pia kuwa mashemasi.
Kuwatawaza wanawake
kama Wachungaji/Wazee/Mashemasi ni ukiukaji wa Neno la Mungu na kwa sababu
ya ukosefu wa ufahamu wa kimaandiko, au ni jaribio la kuifanya Biblia iseme
kile kinachokidhi shauku ya kimwili ya mwanadamu. Hatupaswi kuruhusu shinikizo la kitamaduni au
usahihi au msukumo wa kisiasa kubadili wa kanisa na Mamlaka yake.
Kwa kuwa sifa zilizoorodheshwa katika 1Thimotheo 3 pia inasema kwamba shemasi lazima awe
“mume wa mke
mmoja” (1Tim. 3:2), kwa hiyo ni wazi kwamba ofisi ya shemasi inapaswa
kusimamiwa na wanaume.
Andiko muhimu sana linalohusu nani awe Mzee au Mchungaji ni
hili lifuatalo; 1Timotheo 3:45 “mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye
kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake
mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)” Kifungu hiki kinaunganisha wazi
mamlaka ya mwanaume akiwa nyumbani kwake na mamlaka ya wanaume kanisani. Ni wazi kwamba Mungu pia aliwaweka wanadamu
kuwa wasimamizi wa Kanisa Lake. Mungu
ameweka muundo wake wa mamlaka na ameweka wazi wanaume katika uongozi juu ya
wanawake.
ALICHOTUFUNDISHA
NDUGU BRANHAM:
1. MWANAMKE ANAWEZA KUIMBA, KUSHUHUDIA, KUNENA KWA LUGHA, KUTABIRI, LAKINI SI KUFUNDISHA WALA KUHUBIRI.
“Swali lilikuwa kama mwanamke ana karama ya lugha na
anataka kunena, ninaamini kwamba wakati huo utakapowadia, ana haki ya kunena kwa karama ya lugha, lakini si kuhubiri au kunyakua
mamlaka yoyote. Juu ya wanaume.
Wakati yeye ni mhubiri, bila shaka yeye ni juu ya wanaume.
65-0429E - Kuchagua
Bibi-Arusi
“Mmoja
alitaka kujua ikiwa ni makosa kwa wanawake kushuhudia, au kuimba, au kutoa
ujumbe kwa lugha, kutafsiri jumbe, au unabii katika kanisa.
Hapana, si vibaya;
ni—ilimradi tu ifike mahali katika utaratibu.
Unaona? Kanisa liko katika
utaratibu, na ni wakati tu…Njia halisi, ya kweli ya kufanya hivyo ni kwa wale
wanaonena kwa lugha na vitu au jumbe zinazotolewa kabla ya ujumbe kutoka
mimbarani, kamwe katika wakati huo; maana Roho Mtakatifu anatoka sehemu moja
kwa wakati, kama Paulo alivyonena pale.
Lakini
wanawake wamejaliwa Karama ya unabii, na wamejaliwa kuwa na Karama lugha na
tafsiri, na kila kitu isipokuwa kuwa wahubiri.
Hawapaswi kuwa wahubiri.
Wamekatazwa kuhubiri makanisani (hiyo ni kweli), kuchukua mahali, ama
kuwa mwalimu, ama cho chote kile kanisani.
Lakini kuhusu karama, mwanamke anazo hizo zote, anaweza kuchukua moja au
mojawapo ya karama hizo tisa za kiroho kulingana na 1 Wakorintho 12, na hayuko
chini ya utumwa kwamba ujumbe wake usitokee mahali pake.” 61-1015M - Maswali na
Majibu
2. MWANAMKE HATAKIWI KUKATA NYWELE WALA KUVAMIA MIMBALA
Sasa ninajua ya kwamba ninyi akina mama hamtaki mahubiri ya
namna hii, lakini ewe dada, umekosea kabisa katika yale ufanyayo. Biblia inakukataza kukata nywele zako. Mungu alikupa hizo ziwe badala ya mavazi.
Alikuamuru uziache ziwe ndefu. Ndiyo utukufu wako. Ulipokata nywele zako
ulionyesha ya kwamba umeacha uongozi wa mume wako. Kama vile Hawa ulitoka
ukaziendea njia zako mwenyewe. Mlipata haki ya kupiga kura. Mmeingilia kazi za
wanaume. Mkaacha kuwa wanawake. Mnapaswa kutubu na kumrudia Mungu. Na kama mambo
haya yote hayakuwa mabaya vya kutosha, wengi
wenu mlichukua wazo kwamba mngeweza kuzivamia mimbara na huduma za kanisa
ambazo Mungu ameziweka kwa ajili ya wanaume na wanaume peke yao. Loo!
Nimetonesha kidonda basi sivyo? Vema, nionyesheni mahali pamoja katika Biblia
ambapo Mungu aliwahi kumchagua mwanamke ye yote kuhubiri ama kutwaa mamlaka juu
ya mwanamume, nami nitaomba msamaha kwa yale niliyosema. Hamwezi kupata kwamba
nimekosea. Ninasema kweli, kwa maana ninashikilia Neno na niko kwenye Neno.
Kama mngalikuwa tajiri Kiroho mngejua ya kwamba hiyo ni kweli. Hakuna kweli ila
Neno. Paulo alisema, “Simpi mwanamke
ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume.” Huwezi kamwe kuchukua
nafasi katika zile huduma tano za Efe. 4 bila kuwatawala wanaume. Dada,
afadhali ulisikilize hilo Neno. Haikuwa ni Roho wa Mungu akijidhihirisha katika
maisha yaliyojazwa Roho aliyekwambia uhubiri kwa sababu Roho na Neno ni MMOJA.
Roho na Neno wanasema jambo lile lile. Mtu fulani alifanya kosa. Mtu fulani
alidanganyika. Amkeni kabla hamjachelewa. Shetani alimdanganya Hawa, mama yenu;
anawadanganya binti zake sasa. Mungu na awasaidie.
Maelezo Ya Nyakati Saba Za Kanisa (9 – Wakati wa Kanisa la
Laodikia)
3. MWANAMKE, SI MWANAUME, ALIDANGANYWA KATIKA BUSTAN YA EDEN.
128 Yeye
(Hawa) alimshawishi (Adam) kuacha mapenzi ya Mungu na kumfanya atende jambo
ambalo haikumpasa kutenda, na, kwa hilo, akasababisha mauti kwa jamii yote ya
binadamu. Hiyo ndiyo sababu Biblia
inamkataza kufundisha, ama kuhubiri, ama kushughulikia Neno la Mungu, kwa njia
yoyote.
129 Najua,
kina dada, wengi wenu husema, “Bwana aliniita kuhubiri.”
130 Sitabishana
na wewe. Bali nitakuambia, Neno linasema haikupasi kufanya hivyo.
“Hatafundisha, ama kutwaa mamlaka yoyote, bali yampasa kuwa kimya.”
“Vema,” unasema, “Bwana aliniambia nifanye hivyo.”
131 Silitilii
hilo shaka hata kidogo. Je, mlisikia Ujumbe wangu hivi majuzi usiku kuhusu
Balaamu? Balaamu alipata uamuzi wa
kwanza, waziwazi wa Mungu, “Usitende hayo.” Bali aliendelea kujipumbaza hata
mwishowe Mungu akamwambia aende akatende hayo.
132 Mungu anaweza akakuruhusu kuhubiri.
Sisemi hakufanya hivyo. Bali si
kulingana na Neno Lake la asili pamoja na mpango. “Kwa sababu yampasa awe
mtiifu, kama isemavyo torati.” Ni kweli. Kwa hivyo, hapaswi kufanya hivyo.
65-0429E - Kuchagua Bibi-Arusi
4. ATAOKOLEWA KWA UZAZI WAKE
214 Loo, hivi hamwoni? Hiyo ndiyo sababu Paulo alisema ya kwamba mwanamke kamwe hapaswi kuihubiri Injili. Uh-hum. Alikuwa—alikuwa katika…Yeye ndiye aliyedanganyika. “Simruhusu mwanamke kufundisha, wala kutwaa mamlaka yoyote, bali awe mtulivu.” Mnaona? “Kwa kuwa—kwa kuwa Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. Wala Adamu hakudanganyika, bali mwanamke alidanganywa, akawa makosani.” Kasema, “Hata hivyo, sasa, yeye hajapotea; ataokolewa kwa kuwazaa watoto (kama yuna mume), na kadhalika, akiendelea mbele, imani na kiasi na utakatifu wote pamoja na mambo kama hayo, yeye ataokolewa. Lakini kamwe msimruhusu mmoja kufundisha wala kuchukua mamlaka!” Mnaona? Paulo alisema, “Msifanye hivyo!” Kasema, “Sasa, nafikiri ninayo nia ya Bwana,” akasema.
215 Wao walisema, “Mbona, ninii…Mbona, manabii huko
walitabiri na kutwambia ya kwamba ‘tunapaswa kuhubiri.’”
216 Yeye akasema, “Au
je? Neno la Mungu lilitoka kwenu, na hivi lilikuja kutoka kwenu peke yenu? Kama
mtu yeyote akijiona kuwa ni wa kiroho ama nabii, na atambue ya kwamba yale
nisemayo ni Amri za Bwana.” Mnaona? Hiyo ni kweli. Yeye alijua alichokuwa
akizungumzia.
217 Lakini kasema, “Kama
yeye ni mjinga, acha tu awe mjinga. Hivyo tu. Ha—hatalisikiliza, vema, acha
tu aendelee, yeye anaelekea moja kwa moja shimoni. Mnaona, lakini endelea tu.”
Lakini hapo, hizo roho mbili.
218 Hoja. Kama vile walivyo na wanawake kwenye jeshi la polisi, huko nje mitaani. Hiyo ni fedheha kwa bendera ya Marekani,
kuwaweka hao akina mama huko mtaani. Huku
makumi ya maelfu ya wanaume hawana kazi! Mbona, ni taifa la mwanamke, ni
mahali pa mwanamke, mwanamke atatawala. Ni kuabudiwa kwa mwanamke. Ni ile roho
ya mafundisho ya sharti ya Kikatoliki, kumwabudu mwanamke kama mungu. Hii hapa
hiyo ninii tu…Yote yako tayari, hivi hamwoni huo mpangilio?
219
Hakuna kitu ambacho Mungu angalimpa mwanamume cha
kupendeza kuliko mke, mke halisi. Lakini wakati anapopata kitu kingine zaidi ya
hicho, yeye—yeye yuko nje. Hiyo ni kweli kabisa. Mungu kamwe hawakusudii wanawake kufanya kazi katika yoyote ya sehemu
hizi na kufanya mambo kama hayo. Wanawake hawa, nyinyi ni…inawapasa kuzaa
watoto na kuwalea watoto wao. Wote ni
wahubiri wadogo, kila mmoja wao, bali wana uchungaji wao wenyewe nyumbani
pamoja na watoto wao, wakiwalea watoto wao. Vema.
60-1211M - Wale
Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu
5. MWANAMKE HALISI NI KITO
Kwa hiyo, bali sasa, mwanamke
mzuri ni lulu katika taji ya mwanamume. Anapaswa aheshimiwe. Yeye…Mama
yangu ni mwanamke, mke wangu vile vile, nao ni wazuri sana. Nami ninao maelfu
ya Dada Wakristo ambao ninawaheshimu sana. Bali kama—kama wanaweza kuheshimu
kile Mungu alichowafanya, umama na malkia wa kweli, hilo ni sawa. Mwanamke ni
moja ya mambo mazuri zaidi kuliko yote ambayo Mungu angeweza kumpa mwanamume,
ilikuwa ni mwanamke. Kando ya wokovu,
mwanamke ndicho kitu kizuri zaidi ya vyote kama yeye ni mke mzuri. Bali
iwapo yeye sivyo alivyo, Sulemani
alisema, “Mwanamke mwema ni lulu katika taji ya mwanamume, bali aliye m—mkaidi
au asiyefaa ni maji damuni mwake.” Na hiyo ni kweli, ndilo jambo baya mno
linaloweza kutukia. Kwa hiyo mwanamke mwema…Kama una mke mwema, ndugu, yakupasa kumheshimu sana. Hilo ni kweli,
yakupasa kufanya hivyo. Mwanamke halisi! Pia, enyi watoto, kama mna mama halisi
ambaye hukaa nyumbani akijitahidi kuwatunza, kuwasafishia nguo zenu,
anawapeleka shuleni, akiwafundisha habari za Yesu, yawapasa kumheshimu mama
mzuri huyo mwenye upendo kwa yote yaliyo ndani yenu. Yakupasa kumheshimu
mwanamke huyo, ndiyo, bwana, kwa sababu yeye ni mama halisi.
59-0419A - Hadithi Ya Maisha Yangu
6.KUWA “MWANAMKE MWENYE KUTAWALA” NI MPINGA KRISTO
“Sasa mwanamke
hapaswi kuwa na tabia ya chuma. Yeye, kulingana na Maandiko Matakatifu, anapaswa kuwa mtiifu kwa mwanamume.
Ameamriwa hayo. Mwanamke ambaye kweli ni mwanamke, mwanamke kabisa kabisa,
atakuwa na tabia hiyo. Si jamvi la mlangoni. Hakuna mwanamume halisi
anayemfanya mwanamke jamvi la mlangoni. Lakini atapenda kuwa chini ya mamlaka
na kutokumtawala mwanamume, kwa maana yeye ndiye kiongozi wa nyumba. Kama akivunja mfano huo ambao amewekewa na
Mungu, yeye amepotoka. Mwanamume ye yote anayemruhusu mwanamke achukue
mamlaka naye pia amevunja mfano huo na Yeye
amepotoka. Hiyo ndiyo sababu mwanamke
HAWEZI KUVAA MAVAZI YAMPASAYO MWANAMUME AMA KUKATA NYWELE ZAKE. Hapaswi
kamwe kuvaa mavazi yanayompasa mwanamume wala kukata nywele zake. Wakati
anapofanya hivyo anaingilia mamlaka ya mwanamume akitwaa mamlaka na kujipotosha
mwenyewe. Na mwanamke anapoivamia
mimbara jambo ambalo AMEAMRIWA ASIFANYE, anaonyesha yeye ni wa roho ya namna
gani. Kuwa mtawala mwanamke ni upinga-Kristo na mbegu za Kanisa Katoliki la Kirumi
zimo ndani yake ingawa anaweza kukanusha jambo hili kwa ukali sana. Lakini
INAPOFIKIA KWENYE NENO, Neno la Mungu liwe kweli na kila neno la mwanadamu liwe
uongo. Amina.
Maelezo Ya Nyakati Saba Za Kanisa (6 – Wakati wa Kanisa la
Thiatira)
58 Katika Tucson—katika Tucson, Arizona, tuna mahakimu mwanamke pale mjini. Hiyo
ndiyo sababu mji huo umechafuka sana. Nasi tuna…Mwanamke hana shughuli zo zote katika siasa. Hana shughuli zo zote
katika…juu ya mamlaka yo yote kanisani.
59 Mahali pake ni
malkia wa mwanamume nyumbani. Nje ya jambo hilo, hana kitu. Nasi tunajua
jambo hilo kuwa ni Kweli. Hamtampata…Najua jambo hilo linasikika la mtindo wa
kikale, bali mimi ninawajibika.
60 Nami najua ya kwamba, baada ya kuondoka kwangu kutoka
dunia hii, hizo kanda na vitabu vitaendelea kuwepo, na wengi wenu ninyi watoto
wadogo mtaona, katika siku zijazo, ya kwamba jambo hili ni Kweli kabisa, kwa
maana nanena katika Jina la Bwana.
65-0815 - Nawe Hujui
👉 (English version )Endtimemessage