Ukweli Kuhusu Wanawake Kuhubiri

 


Mungu anawajali wanawake kama vile tu anavyowajali wanaume. Ndiyo, wanawake ni muhimu nyumbani, kanisani, na kwenye jamii kama wanaume walivyo. Katika Kristo, wanawake wana nafasi sawa ya kufurahia baraka za kiroho mbele za Mungu kama wanaume wanavyofurahia.  Hata hivyo, hii haimaanishi kwamba kusiwe na tofauti kimuonekano na kimajukumu baina ya wanaume na wanawake.  Kuna ukweli ambao unahitaji kuwa wazi katika kanisa na jamii leo: Wanaume na wanawake waliumbwa na Mungu kwa namna tofauti! 
KUJUA NAFASI YAKE SAHIHI

Wanaume na wanawake waliumbwa kwa majukumu tofauti. Biblia inathibitisha kwamba wanaume wanapaswa kuwa viongozi nyumbani, kanisa, na serikali. Wanawake hawakuumbwa kutawala taasisi hizi za kimungu; bali wanaume. Hata zile huduma tano katika Waefeso 4:11 ziliundwa kimaandiko kwa ajili ya wanaume, na sio kwa ajili ya wanawake.

Hapo mwanzo, mwanamume na mwanamke walikuwa katika nafasi sawa mbele za Mungu. Lakini wakati Hawa alipoanguka katika kosa baada ya kumsikiliza nyoka, agano lilibadilishwa. Mwanamke huyo sasa alikuwa chini ya utii kwa mwanaume, kama tu inavyojidhihirisha katika Maandiko yafuatayo:

1Thimotheo 2:14-15 “Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa. Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.”

Mwanzo 3:16 “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.”

Waefeso 5:22-24 “Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.”

Nabii Isaya alikuwa akihukumu Israeli wakati aliposema kwamba wanawake wanatawala juu yao (Isaya 3:12). Nabii Eliya pia alikuwa akimhukumu Ahabu kwa sababu mke wake wa kipagani Yezebeli alikuwa akimtawala. Samson aligeuka nje ya mapenzi ya Mungu kwa sababu alisikiliza maagizo ya Delila. Na Adamu mwenyewe alishindwa katika Mungu kwa sababu ya kumsikiliza mkewe Hawa.

Katika kanisa, kulingana na Biblia, hakuna mwanamke anayestahili kuwa mchungaji au shemasi au kushika nafasi nyingine yoyote ya uongozi dhidi ya wanaume. Nani anasema hiyo? Mungu mwenyewe alisema kupitia kinywa chake cha Agano Jipya, mtume Paulo.

1Timotheo 2: 11-15 inasema wazi:

Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna. Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu. Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa. Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.”

1Wakoritho 14:34-37 inasema;

Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo. Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.”

Je! Mwanamke anawezaje kuwa mchungaji wa kanisa wakati yeye amekatazwa kufundisha au kuwa na mamlaka yoyote juu ya wanaume?

Wanawake wanaweza tu kuwa wachungaji ikiwa makanisa yanakataa kwa makusudi na kwa uwazi mafundisho ya Biblia.  Kwa bahati mbaya, makanisa leo, hata Wapentekoste, mara nyingi wameambukizwa na tabia ya kidunia.  Ukombozi wa Wanawake umevamia makanisa (kile wanaita haki sawa).  Kwa hivyo, uasi wa wanawake ulimwenguni unazua matatizo sawa na hayo katika makanisa, na tunapata wanawake wakitamani na kudai nafasi za uongozi katika makanisa mengi.

Mungu ni mwanamume, na kanisa ni mwanamke.  Kwa hiyo, mwanamke anapaswa kumtii mwanamume kama vile kanisa lilivyo chini ya Kristo, na si kinyume chake.

WANAWAKE KATIKA HUDUMA 5?

SUALA KUU linaweza kufupishwa kama ifuatavyo: “Je! Mwanamke anaweza kuwekwa wakfu kwa huduma ya kichungaji?”

Ikiwa unaamini Biblia, jibu ni HAPANA thabiti!

Biblia inazungumza kwa uwazi sana juu ya somo hili bila kuacha nafasi ya uvumi na kuchanganyikiwa, au hata mjadala.  Tatizo ni kwamba makanisa leo mara nyingi sana yanatafuta vyanzo vingine badala ya Biblia ili kuhalalisha imani zao zisizo na maana.  Matokeo yake ni kulewa kwa mawazo yanayopinga mamlaka ya Maandiko.

Ingawa wanawake wanaweza kuhudumu kanisani katika nyadhifa mbalimbali mradi tu uwezo huo haukiuki kanuni za mamlaka na utaratibu na uongozi wa kiume, basi hiyo ni sawa.  Wanawake wanaweza kuwa na mamlaka ya kiroho juu ya wanawake wenzao na watoto lakini si juu ya wanaume.

Sipuuzi ukweli kwamba kuna wanawake wengi ambao wana uwezo mkubwa.  Lakini ni muhimu kukumbuka kuwa suala hili halihusiani na thamani au uwezo.  Inahusiana na maagizo na mamlaka.  Mungu ameweka kitengo cha familia, na Kanisa lenyewe, katika utaratibu ufaao.

1Wakoritho 14:40 inasema; “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.” Waebrania 13:17 Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.”

Wanawake wanaweza kutumika kwa matokeo mazuri kanisani hata hivyo si kama Wachungaji, Wazee au Mashemasi.  Yesu alichagua wanaume kumi na wawili kuwa viongozi wa msingi wa Kanisa Lake, na mitume waliamriwa kuchagua wanaume saba pia kuwa mashemasi.

Kuwatawaza wanawake kama Wachungaji/Wazee/Mashemasi ni ukiukaji wa Neno la Mungu na kwa sababu ya ukosefu wa ufahamu wa kimaandiko, au ni jaribio la kuifanya Biblia iseme kile kinachokidhi shauku ya kimwili ya mwanadamu.  Hatupaswi kuruhusu shinikizo la kitamaduni au usahihi au msukumo wa kisiasa kubadili wa kanisa na Mamlaka yake.

Kwa kuwa sifa zilizoorodheshwa katika 1Thimotheo 3 pia inasema kwamba shemasi lazima awe

mume wa mke mmoja” (1Tim. 3:2), kwa hiyo ni wazi kwamba ofisi ya shemasi inapaswa kusimamiwa na wanaume.

Andiko muhimu sana linalohusu nani awe Mzee au Mchungaji ni hili lifuatalo; 1Timotheo 3:45mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)” Kifungu hiki kinaunganisha wazi mamlaka ya mwanaume akiwa nyumbani kwake na mamlaka ya wanaume kanisani.  Ni wazi kwamba Mungu pia aliwaweka wanadamu kuwa wasimamizi wa Kanisa Lake.  Mungu ameweka muundo wake wa mamlaka na ameweka wazi wanaume katika uongozi juu ya wanawake.

ALICHOTUFUNDISHA NDUGU BRANHAM:

1. MWANAMKE ANAWEZA KUIMBA, KUSHUHUDIA, KUNENA KWA LUGHA, KUTABIRI, LAKINI SI KUFUNDISHA WALA KUHUBIRI.

“Swali lilikuwa kama mwanamke ana karama ya lugha na anataka kunena, ninaamini kwamba wakati huo utakapowadia, ana haki ya kunena kwa karama ya lugha, lakini si kuhubiri au kunyakua mamlaka yoyote.  Juu ya wanaume. Wakati yeye ni mhubiri, bila shaka yeye ni juu ya wanaume.

 65-0429E - Kuchagua Bibi-Arusi

“Mmoja alitaka kujua ikiwa ni makosa kwa wanawake kushuhudia, au kuimba, au kutoa ujumbe kwa lugha, kutafsiri jumbe, au unabii katika kanisa.

Hapana, si vibaya; ni—ilimradi tu ifike mahali katika utaratibu.  Unaona?  Kanisa liko katika utaratibu, na ni wakati tu…Njia halisi, ya kweli ya kufanya hivyo ni kwa wale wanaonena kwa lugha na vitu au jumbe zinazotolewa kabla ya ujumbe kutoka mimbarani, kamwe katika wakati huo; maana Roho Mtakatifu anatoka sehemu moja kwa wakati, kama Paulo alivyonena pale.

Lakini wanawake wamejaliwa Karama ya unabii, na wamejaliwa kuwa na Karama lugha na tafsiri, na kila kitu isipokuwa kuwa wahubiri.  Hawapaswi kuwa wahubiri.  Wamekatazwa kuhubiri makanisani (hiyo ni kweli), kuchukua mahali, ama kuwa mwalimu, ama cho chote kile kanisani.  Lakini kuhusu karama, mwanamke anazo hizo zote, anaweza kuchukua moja au mojawapo ya karama hizo tisa za kiroho kulingana na 1 Wakorintho 12, na hayuko chini ya utumwa kwamba ujumbe wake usitokee mahali pake.” 61-1015M - Maswali na Majibu

2. MWANAMKE HATAKIWI KUKATA NYWELE WALA KUVAMIA MIMBALA

Sasa ninajua ya kwamba ninyi akina mama hamtaki mahubiri ya namna hii, lakini ewe dada, umekosea kabisa katika yale ufanyayo. Biblia inakukataza kukata nywele zako. Mungu alikupa hizo ziwe badala ya mavazi. Alikuamuru uziache ziwe ndefu. Ndiyo utukufu wako. Ulipokata nywele zako ulionyesha ya kwamba umeacha uongozi wa mume wako. Kama vile Hawa ulitoka ukaziendea njia zako mwenyewe. Mlipata haki ya kupiga kura. Mmeingilia kazi za wanaume. Mkaacha kuwa wanawake. Mnapaswa kutubu na kumrudia Mungu. Na kama mambo haya yote hayakuwa mabaya vya kutosha, wengi wenu mlichukua wazo kwamba mngeweza kuzivamia mimbara na huduma za kanisa ambazo Mungu ameziweka kwa ajili ya wanaume na wanaume peke yao. Loo! Nimetonesha kidonda basi sivyo? Vema, nionyesheni mahali pamoja katika Biblia ambapo Mungu aliwahi kumchagua mwanamke ye yote kuhubiri ama kutwaa mamlaka juu ya mwanamume, nami nitaomba msamaha kwa yale niliyosema. Hamwezi kupata kwamba nimekosea. Ninasema kweli, kwa maana ninashikilia Neno na niko kwenye Neno. Kama mngalikuwa tajiri Kiroho mngejua ya kwamba hiyo ni kweli. Hakuna kweli ila Neno. Paulo alisema, “Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume.” Huwezi kamwe kuchukua nafasi katika zile huduma tano za Efe. 4 bila kuwatawala wanaume. Dada, afadhali ulisikilize hilo Neno. Haikuwa ni Roho wa Mungu akijidhihirisha katika maisha yaliyojazwa Roho aliyekwambia uhubiri kwa sababu Roho na Neno ni MMOJA. Roho na Neno wanasema jambo lile lile. Mtu fulani alifanya kosa. Mtu fulani alidanganyika. Amkeni kabla hamjachelewa. Shetani alimdanganya Hawa, mama yenu; anawadanganya binti zake sasa. Mungu na awasaidie.

Maelezo Ya Nyakati Saba Za Kanisa (9 – Wakati wa Kanisa la Laodikia)

3. MWANAMKE, SI MWANAUME, ALIDANGANYWA KATIKA BUSTAN YA EDEN.    

128  Yeye (Hawa) alimshawishi (Adam) kuacha mapenzi ya Mungu na kumfanya atende jambo ambalo haikumpasa kutenda, na, kwa hilo, akasababisha mauti kwa jamii yote ya binadamu. Hiyo ndiyo sababu Biblia inamkataza kufundisha, ama kuhubiri, ama kushughulikia Neno la Mungu, kwa njia yoyote.

129  Najua, kina dada, wengi wenu husema, “Bwana aliniita kuhubiri.”

130  Sitabishana na wewe. Bali nitakuambia, Neno linasema haikupasi kufanya hivyo. “Hatafundisha, ama kutwaa mamlaka yoyote, bali yampasa kuwa kimya.”

“Vema,” unasema, “Bwana aliniambia nifanye hivyo.”

131  Silitilii hilo shaka hata kidogo. Je, mlisikia Ujumbe wangu hivi majuzi usiku kuhusu Balaamu? Balaamu alipata uamuzi wa kwanza, waziwazi wa Mungu, “Usitende hayo.” Bali aliendelea kujipumbaza hata mwishowe Mungu akamwambia aende akatende hayo.

132  Mungu anaweza akakuruhusu kuhubiri. Sisemi hakufanya hivyo. Bali si kulingana na Neno Lake la asili pamoja na mpango. “Kwa sababu yampasa awe mtiifu, kama isemavyo torati.” Ni kweli. Kwa hivyo, hapaswi kufanya hivyo. 65-0429E - Kuchagua Bibi-Arusi

4. ATAOKOLEWA KWA UZAZI WAKE

214   Loo, hivi hamwoni? Hiyo ndiyo sababu Paulo alisema ya kwamba mwanamke kamwe hapaswi kuihubiri Injili. Uh-hum. Alikuwa—alikuwa katika…Yeye ndiye aliyedanganyika. “Simruhusu mwanamke kufundisha, wala kutwaa mamlaka yoyote, bali awe mtulivu.” Mnaona? “Kwa kuwa—kwa kuwa Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa. Wala Adamu hakudanganyika, bali mwanamke alidanganywa, akawa makosani.” Kasema, “Hata hivyo, sasa, yeye hajapotea; ataokolewa kwa kuwazaa watoto (kama yuna mume), na kadhalika, akiendelea mbele, imani na kiasi na utakatifu wote pamoja na mambo kama hayo, yeye ataokolewa. Lakini kamwe msimruhusu mmoja kufundisha wala kuchukua mamlaka!” Mnaona? Paulo alisema, “Msifanye hivyo!” Kasema, “Sasa, nafikiri ninayo nia ya Bwana,” akasema. 

215 Wao walisema, “Mbona, ninii…Mbona, manabii huko walitabiri na kutwambia ya kwamba ‘tunapaswa kuhubiri.’”

216 Yeye akasema, “Au je? Neno la Mungu lilitoka kwenu, na hivi lilikuja kutoka kwenu peke yenu? Kama mtu yeyote akijiona kuwa ni wa kiroho ama nabii, na atambue ya kwamba yale nisemayo ni Amri za Bwana.” Mnaona? Hiyo ni kweli. Yeye alijua alichokuwa akizungumzia.

217 Lakini kasema, “Kama yeye ni mjinga, acha tu awe mjinga. Hivyo tu. Ha—hatalisikiliza, vema, acha tu aendelee, yeye anaelekea moja kwa moja shimoni. Mnaona, lakini endelea tu.” Lakini hapo, hizo roho mbili.

218  Hoja. Kama vile walivyo na wanawake kwenye jeshi la polisi, huko nje mitaani. Hiyo ni fedheha kwa bendera ya Marekani, kuwaweka hao akina mama huko mtaani. Huku makumi ya maelfu ya wanaume hawana kazi! Mbona, ni taifa la mwanamke, ni mahali pa mwanamke, mwanamke atatawala. Ni kuabudiwa kwa mwanamke. Ni ile roho ya mafundisho ya sharti ya Kikatoliki, kumwabudu mwanamke kama mungu. Hii hapa hiyo ninii tu…Yote yako tayari, hivi hamwoni huo mpangilio?

219         Hakuna kitu ambacho Mungu angalimpa mwanamume cha kupendeza kuliko mke, mke halisi. Lakini wakati anapopata kitu kingine zaidi ya hicho, yeye—yeye yuko nje. Hiyo ni kweli kabisa. Mungu kamwe hawakusudii wanawake kufanya kazi katika yoyote ya sehemu hizi na kufanya mambo kama hayo. Wanawake hawa, nyinyi ni…inawapasa kuzaa watoto na kuwalea watoto wao. Wote ni wahubiri wadogo, kila mmoja wao, bali wana uchungaji wao wenyewe nyumbani pamoja na watoto wao, wakiwalea watoto wao. Vema.

   60-1211M - Wale Wanawali Kumi, Na Wayahudi Mia Na Arobaini Na Nne Elfu

5. MWANAMKE HALISI NI KITO

Kwa hiyo, bali sasa, mwanamke mzuri ni lulu katika taji ya mwanamume. Anapaswa aheshimiwe. Yeye…Mama yangu ni mwanamke, mke wangu vile vile, nao ni wazuri sana. Nami ninao maelfu ya Dada Wakristo ambao ninawaheshimu sana. Bali kama—kama wanaweza kuheshimu kile Mungu alichowafanya, umama na malkia wa kweli, hilo ni sawa. Mwanamke ni moja ya mambo mazuri zaidi kuliko yote ambayo Mungu angeweza kumpa mwanamume, ilikuwa ni mwanamke. Kando ya wokovu, mwanamke ndicho kitu kizuri zaidi ya vyote kama yeye ni mke mzuri. Bali iwapo yeye sivyo alivyo, Sulemani alisema, “Mwanamke mwema ni lulu katika taji ya mwanamume, bali aliye m—mkaidi au asiyefaa ni maji damuni mwake.” Na hiyo ni kweli, ndilo jambo baya mno linaloweza kutukia. Kwa hiyo mwanamke mwema…Kama una mke mwema, ndugu, yakupasa kumheshimu sana. Hilo ni kweli, yakupasa kufanya hivyo. Mwanamke halisi! Pia, enyi watoto, kama mna mama halisi ambaye hukaa nyumbani akijitahidi kuwatunza, kuwasafishia nguo zenu, anawapeleka shuleni, akiwafundisha habari za Yesu, yawapasa kumheshimu mama mzuri huyo mwenye upendo kwa yote yaliyo ndani yenu. Yakupasa kumheshimu mwanamke huyo, ndiyo, bwana, kwa sababu yeye ni mama halisi.

59-0419A - Hadithi Ya Maisha Yangu

6.KUWA “MWANAMKE MWENYE KUTAWALA” NI MPINGA KRISTO

“Sasa mwanamke hapaswi kuwa na tabia ya chuma. Yeye, kulingana na Maandiko Matakatifu, anapaswa kuwa mtiifu kwa mwanamume. Ameamriwa hayo. Mwanamke ambaye kweli ni mwanamke, mwanamke kabisa kabisa, atakuwa na tabia hiyo. Si jamvi la mlangoni. Hakuna mwanamume halisi anayemfanya mwanamke jamvi la mlangoni. Lakini atapenda kuwa chini ya mamlaka na kutokumtawala mwanamume, kwa maana yeye ndiye kiongozi wa nyumba. Kama akivunja mfano huo ambao amewekewa na Mungu, yeye amepotoka. Mwanamume ye yote anayemruhusu mwanamke achukue mamlaka naye pia amevunja mfano huo na Yeye amepotoka. Hiyo ndiyo sababu mwanamke HAWEZI KUVAA MAVAZI YAMPASAYO MWANAMUME AMA KUKATA NYWELE ZAKE. Hapaswi kamwe kuvaa mavazi yanayompasa mwanamume wala kukata nywele zake. Wakati anapofanya hivyo anaingilia mamlaka ya mwanamume akitwaa mamlaka na kujipotosha mwenyewe. Na mwanamke anapoivamia mimbara jambo ambalo AMEAMRIWA ASIFANYE, anaonyesha yeye ni wa roho ya namna gani. Kuwa mtawala mwanamke ni upinga-Kristo na mbegu za Kanisa Katoliki la Kirumi zimo ndani yake ingawa anaweza kukanusha jambo hili kwa ukali sana. Lakini INAPOFIKIA KWENYE NENO, Neno la Mungu liwe kweli na kila neno la mwanadamu liwe uongo. Amina.

Maelezo Ya Nyakati Saba Za Kanisa (6 – Wakati wa Kanisa la Thiatira)

58 Katika Tucson—katika Tucson, Arizona, tuna mahakimu mwanamke pale mjini. Hiyo ndiyo sababu mji huo umechafuka sana. Nasi tuna…Mwanamke hana shughuli zo zote katika siasa. Hana shughuli zo zote katika…juu ya mamlaka yo yote kanisani.

59   Mahali pake ni malkia wa mwanamume nyumbani. Nje ya jambo hilo, hana kitu. Nasi tunajua jambo hilo kuwa ni Kweli. Hamtampata…Najua jambo hilo linasikika la mtindo wa kikale, bali mimi ninawajibika.

60 Nami najua ya kwamba, baada ya kuondoka kwangu kutoka dunia hii, hizo kanda na vitabu vitaendelea kuwepo, na wengi wenu ninyi watoto wadogo mtaona, katika siku zijazo, ya kwamba jambo hili ni Kweli kabisa, kwa maana nanena katika Jina la Bwana.

65-0815 - Nawe Hujui

  👉 (English version )Endtimemessage

       Pakua pdf 👈


 




Previous Post Next Post