VPN

VPN ni nini?


VPN inasimama badala ya Virtual Private Network. Ni kama handaki maalum kwenye wavuti linaloweza kuficha data/taarifa zozote unazotuma au kupokea ukiwa unaperuzi mtandaoni. Hii inaweka taarifa zako kuwa siri/faragha kutoka kwa mtoa huduma wa mtandao yaani Internet Service Provider (ISP), watoa huduma za matangazo wanaotaka kufuatilia historia ya vitu unavyovitazama mtandaoni vile vile watu wabaya wanaotaka kuiba taarifa zako binafsi. VPN inaweza pia kufanya uonekane kuwa uko kwenye eneo lingine tofauti na ulilo wakati ukiperuzi mtandaoni mfano kwa kutumia VPN unaweza kuonekana uko Arusha wakati huo uko Lusaka.

Hapo zamani, makampuni ndiyo yalikuwa yakitumia zaidi huduama ya VPN ili kulinda taarifa/data zao zilizopo mtandaoni, lakini hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la huduma za VPN kwa matumizi ya kibinafsi, kwa maana hata watu binafsi wameanza kutumia huduma ya VPN kwa kiasi kikubwa. Mifano mizuri ni kama kuunganisha Wi-Fi za jumuiya au kuhakikisha taarifa za kifedha zinakuwa salama kwenye wavuti.

Unaweza kutumia VPN kwenye kompyuta yako, Tablet, Simu janja, Runinga janja, au kwenye ruta (router). Kwenye kila mojawapo ya vifaa hivyo, kutumia VPN inaweza kukusaidia usijulikane (anonymous) kwa kuficha eneo ulilopo muda ukiwa mtandaoni na inaongeza usalama hasa pale unapounganisha Wi-Fi ya umma/jumuiya.

Ili kutengeneza muunganisho huu salama, utahitaji kutumia programu tumishi kwenye kompyuta yako inayoitwa VPN client, ambayo inaunganisha kompyuta yako na seva ya VPN katika eneo lingine. Trafiki yote kati ya kompyuta yako na seva inakuwa iko (encrypted) imesimbwa, kuzuia watu wengine wasione taarifa/data ambayo una-share (unashiriki).

VPN Protocol: Hii ni teknolojia ambayo VPN hutumia kutuma na kupokea taarifa wakati huo inazuia mtu yeyote kujua hasa taarifa hiyo ni nini. Kila VPN protocol hutumia sheria na utaratibu tofauti kuwasiliana kati ya kompyuta yako na seva ya VPN. Baadhi zinazingatia suala la salama zaidi, wakati zingine zinazingatia uharaka na zingine ubora hivyo zote huwa zinakuwa na kusudi Fulani.

Seva ya VPN: Ni kompyuta kubwa yenye nguvu iliyopo sehemu tofauti na ilipo kompyuta yako na inaunganishwa na kopyuta yako kupitia VPN. Watumiaji wengine pia wanakuwa wameunganishwa na kompyuta hii wakati huo huo. Unapotembelea ukurasa wa wavuti kwenye kompyuta yako, VPN hutuma ombi kwenye seva ya VPN, halafu wavuti huona ombi kana kwamba inatoka kwa seva badala ya kutoka kwako. Hivi ndivyo unavyoweza kujifanya uko katika nchi nyingine au eneo lingine. Mtoa huduma ya VPN mwenye seva nyingi zaidi, na zilizopo maeneo mengi zaidi, husaidia VPN kufanya kazi haraka kwani unashiriki kompyuta yenye nguvu na watumiaji wengine wachache.

IP Adress: hii ni anwani yako ya mtandaoni ya kifaa chako ambayo hutumiwa na tovuti kutuma data/taarifa ulizoziomba. Anwani yako ya IP inaweza kujumuisha taarifa juu ya eneo ulilopo, aina ya kifaa unachotumia, na hata maelezo kama vile kivinjari unachotumia.

Static/Ddicated IP: ni kama kuwa na anwani maalum ya IP kila wakati unapounganisha kupitia VPN yako. Bila hiyo, anwani yako ya IP inaweza kubadilika kila unapoingia mkondoni. Kuwa na aina hii ya IP inasaidia kuzuia changamoto zinazowez kujitokeza kwa kutumia IP moja na watu wengine mfano  anwani (shared) iliyoshirikiwa inaweza kufungwa kwa sababu ya tabia mbaya ya baadhi ya watumiaji wengine.

 VPN inafanyaje kazi?

VPN inafanya kazi ya kuziweka taarifa zako kwa mfumo wa code (encrypt) na kisha kuzificha kwenye kitu mfano wa handaki kisha kuzisafirisha kutoka eneo moja hadi jingine. VPN inaweza pia kukufanya uonekane kama uko kwenye eneo lingine kwa kutumia seva ambayo iko tofauti na eneo ulilopo muda huo unatumia mtandao.

Unapotumia VPN, kwenye kifaa chako inafanya kazi ya (ku-encrypt) kusimba shughuli zote unazouwa unazifanya kwenye mtandao au kabla ya kutuma taarifa zako kwa njia ya mtandao. Kwa kutumia VPN taarifa zako zitafungwa (encrypted) na zitasafirishwa kwa namna ya faragha. Wakati kwa upande mwingine yaani taarifa zinakoenda, seva ya VPN katika eneo tofauti itazifungua (decrypt) taarifa hizo baada ya kufika, na baada ya hapo, seva hutuma ombi lako kwa wavuti au huduma ya utiririshaji. Once a Baada ya maobi yako kurejeshwa, seva inazifungua (decrypt) taarifa zako ten ana kisha kuzituma kwenye kifaa chako mfano simu au kompyuta.

Wakati seva inatuma taarifa yako, wavuti au huduma inapoona anwani ya IP ya seva inayopokea taarifa, kwa hivyo anwani yako ya IP inawekwa faragha. Anwani ya IP huwa inabeba taarifa kama vile eneo la jiografia ya kompyuta yako, kwa kifupi eneo ulilopo ukiwa unavinjari mtandaoni pia huwa na taarifa za kivinjari (brawser) gani unatumia, Pamoja na taarifa zingine ambazo zinaweza kukutambulisha. Kwa kutumia anwani tofauti ya IP pia huzuia wengine kujiunganisha shughuli zako za kimtandao.

Mara nyingi, utatumia huduma ya VPN moja kwenye kila kifaa chako, lakini kuna huduma kadhaa za VPN zinazofanya kazi kwenye router yako ya Wi-Fi. Kuweka VPN kwenye router yako inafanya iwe rahisi kuunganisha vifaa vyote nyumbani kwako na VPN bila programu binafsi (kwa maana kwenye kila kifaa). Hii inafaida kuu mbili: Kwanza, inakuruhusu kuunganisha vifaa zaidi ya kimoja na kwa wakati mmoja kwani watoa huduma za VPN kawaida huhesabu router kama kifaa kimoja. Pili, inaunganisha Televisheni janja, vifaa vya mchezo (games), vifaa vya utiririshaji, Monita za watoto, na kifaa chochote chenye uwezo wa kuunganishwa na Wi-Fi kwa VPN.

Ni muhimu kupata VPN ambayo inasaidia muunganisho wa wakati mmoja ili uweze kuunganisha kompyuta yako ndogo, Tablet, na simu yako wakati kwa wakati mmoja, badala ya kuwa na VPN kwa kila kifaa.

Kutokana na vyanzo mbali mbali hii ndio orodha ya VPN bora kwa waka 2020 ExpressVPN, PrivateVPN, NordVPN, Windscribe, Private Internet Access, CyberGhost, Surfshark, TunnelBear, IPVanish, ProtonVPN

Vile vile kama unahitaji VPN ya bure unaweza kutazama moja ya hizi hapa Windscribe, Tunnelbear, ProtonVPN

 

 

 


Previous Post Next Post